Mshauri Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Itikadi na Uenezi wa Chama hicho, Salim Bimani wametuhumiwa kufanya Mkutano bila kibali mnamo Desemba 2019, huko Micheweni Zanzibar
Hata hivyo, Viongozi hao wameachiwa kwa dhamana na Chama chao kupitia Mtandao wa Twitter kimedai walifanya Mkutano wa ndani usiohitaji kibali
Viongozi hao waliripoti Polisi asubuhi ya leo kuitikia wito wa Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (RCO) wa Mkoa wa Kaskazini Pemba