Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan ameridhia ujenzi wa barabara ya Kibada- Mwasonga-Kimbiji , ya kilomita 51 kujengwa kwa kiwango cha lami.
Kauli hiyo imetolewa Jijini Dar es salaam leo na Waziri wa Ujenzi, Inocent Bashungwa katika ziara yake kwa mkoa wa Dar es Salaam kwa ajili ya kukagua miundombinu ya barabara iliyoharibiwa na mvua.
“Rais wetu baada kumpelekea taarifa ya changamoto ya barabara hii awali iliyoridhiwa kujengwa kwa kilomita 41,Rais ameongeza ujenzi huo uwe wa kilomita 51,” amesema.
Amesema hatua iliyopo kwa sasa ni mkandarasi kupeleka mitambo ili mvua zitakapoisha aande ujenzi wa barabara hiyo mara moja.
Akizumngumzia mji wa Kigamboni amesema muhimu kwa sababu ni wa kibiashara na unatoa mchango mkubwa hivyo aliwataka wananchi wa Kigamboni kutambua mvua zikiacha watajenga barabara zaa kudumu.
Amesema Serikali imejipanga kufanya tathmini kuwa mvua zitakapoisha kurudisha miundombinu ya barabara ya kudumu hivyo hakuna miundombinu itakayoharibiwa na mvua isirudishwe mawasiliano yake.
” Nimekuja kufanya ukaguzi wa barabara zilizoharibiwa na mvua na kurudisha zoezi la uriudishaji wa mawasiliano ya muda ili kuwezesha shughuli za uzalishaji uchumi kuemndelea na mvua zikiisha tutaendelea na matengenezo ya kudumu ya miundombinu hii.
” Hakuna barabara yoyote itakayokatika mawasiliano serikali ikashindwa kuyarejesha kwa sababu Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ameiwezesha Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kwa ajili ya kurudisha miundombinu iliyoharibiwa na mvua,” amesema.
Amesema maeneo yeyete yenye mikwamo serikali iatawapeleka wakandarasi kurekebisha kwa haraka iwezekanavayo.
Pia amesema Rais Dk. Samia ameridhia ujemnzi wa barabara ya Kibada- Mwasonga-Kimbiji , ya kilomita 51 kujengwa kwa kiwango cha lami.
“Rais wetu baada kumpelekea taarifa ya changamoto ya barabara hii awali iliyoridhiwa kujengwa kwa kilomita 41,Rais ameongeza ujenzi huo uwe wa kilomita 51,” amesema.
Amesema hatua iliyopo kwa sasa ni mkandarasi kupeleka mitambo ili mvua zitakapoisha aande ujenzi wa barabara hiyo mara moja.
Akizumngumzia mji wa Kigamboni amesema muhimu kwa sababu ni wa kibiashara na unatoa mchango mkubwa hivyo aliwataka wananchi wa Kigamboni kutambua mvua zikiacha watajenga barabara zaa kudumu.